Wednesday 13 February 2013



Wanafunzi wa shule ya sekondari ya mchepuo wa kilimo ya Balang’dalalu ya mchepuo wa kilimo iliyopo Wilaya ya Hanang’ Mkoa wa Manyara,wakipalilia mahindi kwenye shamba la shule yao,kama walivyokutwa ijumaa iliyopita ambapo hujilimia wenyewe kwa chakula chao.Picha na Joseph Lyimo


Wanafunzi wa shule ya sekondari Balang’dalalu ya mchepuo wa kilimo iliyopo Wilaya ya Hanang’ Mkoa wa Manyara,wakipalilia mahindi kwenye shamba la shule yao ambapo hujilimia wenyewe kwa chakula chao.

MTOTO WA AJABU ANAYE PUMUA MOTO NA KUPOTEA GHAFLA.

Bi Ann Feria Santos wa nchini Colombia amechanganyikiwa na kuingia na woga baada ya kujifungua mtoto wa ajabu akidai kuwa anapumua moto na kutema cheche.
Ann mwenye umri wa miaka 28, analalamika akieleza kwamba kichanga chake cha kiume chenye umri wa miezi miwili kuwa ni mtoto wa shetani.

Ann aliyasema hayo baada ya mtoto huyo kuchoma godoro na nguo kisha kutoweka katika kitanda chake, mahali alipokuwa amemlaza.
Alilalamika kuwa mtoto huyo amekuwa akitengeneza moto na kuchoma vifaa vyake mbalimbali na samani za nyumbani.

Anasema kuwa mtoto huyo pia amekuwa akijibadilisha mara kwa mara na kuwa na macho ya ajabu yanayowafanya watu kumwogopa kila wanapomwona.
Ann anasema kuwa wakati mwingine husikia mtoto huyo akicheka kwa sauti za ajabu na kutisha.

Anasimulia kuwa njia mojawapo aliyotumia kusitisha sauti hizo za ajabu ni kumtaka anyamaze, ambapo mtoto huyo amekuwa akitii na kukaa kimya.
"Mara nyingi anaweza akapotea tu. Nimemlaza ndani, lakini nikienda kumwangalia nakuta hayupo. Hata nikijaribu kumwangalia simwoni tena, ila ukiondoka, baadaye anarudi na akiamka anaanza kulia kwa sauti. Hapo namchukua na kumpa maziwa,”anasema Ann.
Tatizo hilo limempata Ann kutoka jamii ndogo ya Nueva Estrella, huko Colombia katika ukanda wa Caribbean na kwa kiasi kikubwa jamii ya ukanda huo inaamini ushirikina.
Lakini mama huyo wa watoto watano, anaendelea kumtunza mtoto wake ingawa anakumbana na vikwazo vya mara kwa mara.

Alipozungumza na jarida la The Sun Ann la nchini Uingereza, Ann alisema: "Huyu ni mtoto wa kishetani. Sijawahi kuona mtoto kama huyu katika maisha yangu yote, lakini siwezi kumtupa kwani nimemzaa na nilitunza mimba kwa miezi tisa."

Anasema kuwa mtoto wake aliwahi kupotea kutoka katika familia yake na kwa wakati huo alikuwa katika kitanda cha mbao, lakini akaonekana katika mazingira yasiyo ya kawaida.
Mtoto huyo pia amewahi kukutwa katika bakuli, friji, mashine ya kufulia nguo, hata katika begi lililotundikwa ukutani.
"Begi lingeweza kudondoka ikiwa lingewekwa ndizi 20 tu, lakini inashangaza kwa uzito alionao mtoto na begi hilo halikudondoka wala kuonyesha dalili za kujawa kitu kizito,” anasema.
Ann alionyesha kabati na kusema: "Nilimwona ameketi juu ya kabati lile akionekana na ukubwa kama mtoto wa mwaka mmoja. Alikuwa na macho ya kutisha sana pamoja na pembe zilizoota kichwani."

Maelezo ya Ann yanashabihiana na filamu ya ‘The Omen’ iliyotengenezwa mwaka 1976, ambapo mtoto aliyeitwa Damien alikuwa na maajabu kama aliyonayo mtoto huyo.
Mtoto huyo alivyoonekana akilia mbele ya mwandishi wa habari huku akitoa sauti ya ajabu, lakini tofauti na maelezo ya Ann, hakuna pembe yoyote iliyoonekana kichwani .

Wenyeji wa kijiji anachoishi Ann na mtoto huyo, mara nyingi wamekuwa wakirusha mawe katika nyumba yake wakimtaka amtoe nje mtoto wake ili wampoteze, jambo ambalo mama huyo analipinga vikali.

Hata hivyo, baadhi ya watu wanalalamika wakidai kuwa mama huyo amefuga mauzauza.
Kwa maelezo hayo, huenda Ann akaingia kwenye rekodi mbaya ya unyanyasaji wa watoto kwa kuwa madaktari wanakanusha maneno yake, wakieleza kuwa kulingana na vipimo vya kitabibu, mtoto huyo ni wa kawaida kama walivyo wengine.
 

WAZIRI MKUU MK PINDA AWASHAWISHI WADAU KUWAJALI WATOTO




WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda amewataka wadau mbalimbali yakiwemo mashirika kujikita katika kuyasaidia makundi yasiyojiweza wakiwamo watoto waishio mazingira magumu.

Aliyasema hayo juzi alipotembelea Kituo cha Kulelea Watoto Yatima cha SOS Children’s Village kilichopo eneo la Ngaramtoni wilayani Arumeru, mkoani Arusha na kujionea hali halisi ya kituo hicho. Alisema kumekuwapo na ongezeko kubwa la watoto wanaoishi katika mazingira magumu wanaotokea katika maeneo mbalimbali hali ambayo imekuwa ikisababishwa na walezi ama wazazi wao kutokana na migogoro katika familia na kusababisha watoto wengi kutoroka nyumbani na kuishia mitaani.

Alisema kutokana na hali hiyo kumekuwapo na idadi kubwa ya watoto ambao wamekuwa wakilelewa katika vituo mbalimbali na kupatiwa huduma za kijamii. Pinda katika kuona umuhimu wa kituo hicho pamoja na changamoto mbalimbali zinazowakabili alichangia Sh60 milioni kusaidia kutatua changamoto mbalimbali kituoni hapo.

Naye Mwenyekiti wa Kampuni ya Modern Holdings (EA) Limited Anselm Minja ambaye alimuunga mkono waziri mkuu kwa kuchangia Sh10 milioni.
Pupils of King’ong’o Primary School in Nyeri study in class last year. Presidential candidates promised to offer free primary and secondary education if elected but failed to outline the details of how they will achieve such a feat of reforming the education sector already plagued by complex and myriad problems ranging from teacher underpayment, teacher shortage, poor compensation, declining quality of learning in primary schools among many others. FILE/NATION


In Summary: 1st ever KENYAN PRESIDENTIAL DEBATE FEBRUARY 2013
  • Sparked by a question from a teacher, Ms Irene Omangi, the debate on education dwelt on teacher shortage, poor compensation, declining quality of learning in primary schools in light of free primary education, relevance of the curriculum and the large numbers of children routinely locked out of secondary education

Wednesday 19 September 2012

ULEMAVU SI MWISHO WA MAISHA YA MAFANIKIO



















MTOTO ALIYEZALIWA NA ULEMAVU WA VIUNGO AKIWA NA NDUGU JAMAA NA MARAFIKI WAKIFURAHI PAMOJAMAISHA YANATEGEMEA SANAA NA JINSI UNAVYOPOKEA CHANGAMOTO ILIYOKO MBELE YAKO KWA MTAZAMO CHANYA KATIKA MAZINGIRA HASI. KINACHOHITAJIKA NI KUONA KINACHOWEZEKANA KATIKA KISICHOWEZEKANA ILI KUKABILI MAISHA NA KUISHI MAISHA YA AMANI NA MAFANIKIO.